Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Kuoga katika sheria lina hekima na faida nyingi, miongoni mwa hizo ni kama zifuatazo :

1. Kupata thawabu

Hii ni kwa sababu Kuoga kwa maana na mtazamo wa kisheria ni Ibaada kwa kuwa ndani yake kuna kutekeleza amri ya sheria na kuitumia hukumu ya sheria.

Kwa hivyo lina hili la utekelezaji amri na hukumu ya sheria ujira mkubwa.

Ni kwa mantiki hii ndio Bwana Mtume akatuambia :

 

الطُّهُورُ شَطْرُ الْإِيمَانِ]    رواه مسلم]

 

[Twahara ni nusu ya imani]     [Imepokelewa na Muslim.]

Ni vema ikaeleweka wazi kuwa twahara imekusanya udhu, Kuoga, Tayammum na mengineyo.

2. Kuwa Msafi

Muislamu anapokoga, mwili wake hutakasika na kuwa msafi.

Usafi huu ni kinga kubwa ya vijidudu vinavyoweza kusababisha maradhi kama vile upele na humfanya muislamu anukie vema, kitu ambacho humkurubisha na watu kwani watu humteta mtu mchafu anukaye.

Imepokelewa kutoka kwa Bibi Aisha Allah amuwie radhi kwamba amesema :

 

كان أصحاب رسول الله صلى الله عليه وسلم عمال أنفسهم، وكان يكون لهم أرواح، فقيل لهم: لو اغتسلتم.]   متفق عليه]

 

[Maswahaba wa Bwana Mtume ﷺ walikuwa wakijifanyia kazi wenyewe (na hawakuwa na watumishi) wakawa na harufu mbaya ya jasho. Wakaambiwa na Mtume

[Lau mngalikuwa mnakoga].    [Imepokewa na Bukhari na Muslim]

Na katika upokezi mwingine Mtume ﷺ Amesema:

 

[لو اغتسلتم يوم الجمعة]

 

[Lau mngalikuwa mnajitwahirisha kwa ajili ya siku ya Ijumaa].

3. Kuwa mchangamfu na kupata nguvu.

Mwili wa mwanadamu anapokoga huwa na nguvu mpya na kurudia kuwa katika hali ya uchangamfu baada ya ulegevu na uchovu ambao humsababisha uvivu na kutokujisikia kufanya jambo lolote zaidi ya kubweteka bwete!

Hili la kujisikia kuchoka na mwili kunyong’onyea hupatikana zaidi mara tu baada ya tendo la kujamiiana.

Kwa maneno ya jumla, Hikma ya kuoga kwa ajili ya twahara na usafi humuandaa mtu na kumuweka katika nafasi nzuri ya kuwasiliana na kuzungumza na Mola Muumba wake ndani ya swala akiwa katika hali njema kabisa.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6575111
TodayToday3178
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 8

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68292eacd3e0f3800299341747529388
title_68292eacd3f6e7411854271747529388
title_68292eacd410116770196831747529388

NISHATI ZA OFISI

title_68292eacd62bc9194100731747529388
title_68292eacd641115363953591747529388
title_68292eacd65559595469331747529388 Add content here

HUDUMA MPYA

: 8 + 9 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com