Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Kwanza: Maji Yenye kutwahirisha

1. Maji ya Kawaida:

Nayo ni maji ambayo yamebaki katika sifa yaliyoumbiwa nayo, kama maji yanayoteremka kutoka mawinguni, kama vile mvua, theluji na mvua ya barafu au yenye kutembea ardhini, kama maji ya bahari, mito na maji ya mvua na maji ya visima. Mwenyezi Mungu Mtukufu Anasema

 

وَأَنزَلْنَا مِنَ السَّمَاءِ مَاءً طَهُورًا}    الفرقان:48}

 

[Na tumeyateremsha kutoka mbinguni maji safi]    [25: 48]

Mwenyezi Mungu Mtukufu Amesema:

 

وَيُنَزِّلُ عَلَيْكُم مِّنَ السَّمَاءِ مَاءً لِّيُطَهِّرَكُم بِهِ}     الأنفال:11}

 

[Na akakuteremshieni maji kutoka mbinguni ili kukusafisheni kwayo]    [8: 11]

 

Na Mtume alikuwa akiomba na kusema:

 

  اللهم اغسل خطاياي بالماء والثلج]    رواه البخاري ومسلم]

 

[Ewe Mola wangu! Nitakase na makosa yangu kwa theluji, maji na barafu]   [ Imepokewa na Bukhari na Muslim].

Na alisema tena kuhusu maji ya bahari:

 

هُوَ الطَّهُورُ مَاؤُهُ الْحِلُّ مَيْتَتُهُ]    رواه أحمد أبوداود]

 

[Maji yake ni yenye kutwahirisha na mfu wake ni halali]       [Imepokewa na Ahmad na Abu Daud.]

 

2. Maji yaliyotumiwa:

Nayo ni maji yanayotiririka kutoka kwenye viungo vya mwenye kutawadha au mwenye kuoga. Hayo si makosa kuyatumia kujitwahirishia,

 

عن ابن عباس قال اغتسل بعض أزواج النبي صلى الله عليه وسلم في جفنة فأراد رسول الله صلى الله عليه وسلم أن يتوضأ منه فقالت يا رسول الله إني كنت جنبا فقال إن الماء لا يجنب

Kutoka kwa Ibn Abbas Radhi za Allah ziwe juu yake  kuwa alisema kuwa mmoja katika wake wa Mtume alioga kwenye chombo, na Mtume wa Mwenyezi Mungu akataka kutawadha kutoka kwenye chombo hicho. Yule mkewe akasema: «Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu! Mimi nilikuwa na janaba.” Akasema: [Maji hayaathiriki na Janaba]    [Imepokewa na Tirmidhi.].

 

3. Maji Yaliyochanganyika na kitu Twahara:

Nayo ni maji yaliyochanganyika na kitu twahara kama majani ya mti au mchanga au kutu kwenye matanki ya maji na kisiache athari kwenye yale maji yenye kuyafanya yasiitwe maji ya kawaida. Kwa kauli ya mtume kuwaambia wanawake waliosimama kumshughulikia binti yake aliyekuwa amekufa (Nae ni bi ruqiya Radhi za Allah ziwe juu yake):

 

 اغسلنها ثلاثا أو خمسا أو أكثر من ذلك إن رأيتن ذلك بماء وسدر واجعلن في الآخرة كافورا أو شيئا من كافور]    رواه البخاري ومسلم]

 

[Mwosheni mara tatu au nne au zaidi ya hizo kama itahitajika, kwa maji na majani ya mkunazi, na mwishoni mwake kafuri]      [Imepokewa na Bukhari na Muslim]


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6575041
TodayToday3108
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 18

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_682920522ecbf3412448801747525714
title_682920522ee042480342491747525714
title_682920522ef4012374600931747525714

NISHATI ZA OFISI

title_6829205230f7e10037581331747525714
title_68292052310a911315027741747525714
title_68292052311cf3535101861747525714 Add content here

HUDUMA MPYA

: 4 + 11 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com