Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Kwanini ukaitwa usiku wa cheo (usiku waheshima)?

 Wanachuoni wameeleze sababu ya kuitwa usiku huu wa Laylayul na miongoni mwa sababu walizozitaja ni haya yafuatayo
1. Kumesemwa: Ni kwasababu ya kuutukuza, kama ilivyo katika kauli yake  Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 

وَمَا قَدَرُوا اللَّهَ حَقَّ قَدْرِهِ}    الأنعام:91}

 

[Na (Mayahudi ) hawakumhishimu Mwenyezi Mungu kama inavyotakiwa kumhishimu]  [Al-An-a’m – Aya 91].

Na maana yake: Ni kwamba huu usiku ni wenye hishima; kwa kuteremshwa Qur’ani ndani yake na kupatika na kushuka malaika, na ni usiku wa baraka na rehema na msamaha kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

2. Inasemekana: Al-qadr kwa maana ya kubanika kwa kuwa ndogo sana, kama kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 

وَمَن قُدِرَ عَلَيْهِ رِزْقُهُ فَلْيُنفِقْ مِمَّا آتَاهُ اللَّهُ}    الطلاق:7}

 

[Na yule ambaye amepungukiwa riziki yake (riziki yake imebanika kwa kuwa ndogo sana), atoe katika kile alichopewa na Mwenyezi Mungu]   [At-twalaq – Aya 7].

Na maana ya kubanika kwa kuwa ndogo sana: Ni kule kufichika katika elimu za watu kutambua hasa usiku huo ni usiku wa tarehe ngapi.

3. Na inasemekana: Al-qadr kumaanisha makadirio, kwa maana: katika usiku huu ndiyo kunakadiriwa hukumu za mwaka ulioko; kwa kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 

إِنَّا أَنزَلْنَاهُ فِي لَيْلَةٍ مُّبَارَكَةٍ ۚ إِنَّا كُنَّا مُنذِرِينَ  فِيهَا يُفْرَقُ كُلُّ أَمْرٍ حَكِيمٍ}    الدخان 3-4}

 

[Hakika tumekiteremsha katika usiku ulio barikiwa. Hakika Sisi ni Waonyaji.Katika usiku huu hubainishwa kila jambo la hikima,] [Ad-Dukhan – Aya 3-4].


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6575051
TodayToday3118
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 10

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_682923fb131cb18966383611747526651
title_682923fb1332c891753561747526651
title_682923fb1347618078294381747526651

NISHATI ZA OFISI

title_682923fb156ff11800875451747526651
title_682923fb1584d704645831747526651
title_682923fb159927282378861747526651 Add content here

HUDUMA MPYA

: 4 + 15 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com