Menu

 

 

JE YAFAA KUMUOMBEA DUA KAFIRI ANAEPENDA UISLAMU ??

 

 Suali: Mtu akiwa si muislamu lakini anapenda uislamu na waislamu na kuwataja vizuri. Je mtu huyu akifa inafaa kumuombea dua?

Jawabu: Mtu akiwa hakupiga shahada ya kushuhudia kuwa Mwenyezi mungu ni mmoja na kuwa Mtume muhammad ni Mtume wa Mwenyezi mungu huwa bado hajakuwa Muislamu hata kama alikuwa akijua kuwa uislamu ni dini ya haki,au ni dini yenye mafunzo mazuri, hilo halimfanyi kuwa ni muislamu.
Huyu hapa Ammi yake Mtume ﷺ alikuwa akijua kuwa Uislamu ni dini bora,na aliwahi kutunga mashairi ya kuusifu Uislamu,lakini yeye hakusilimu kwa kuogopa lawama za watu,na alipo kufa Allah Subhana wataala alimkataza Mtume kumuombea msamaha kwa sababu alikufa kafiri Allah anasema:

مَا كَانَ لِلنَّبِيِّ وَالَّذِينَ آمَنُوا أَن يَسْتَغْفِرُوا لِلْمُشْرِكِينَ وَلَوْ كَانُوا أُولِي قُرْبَىٰ مِن بَعْدِ مَا تَبَيَّنَ لَهُمْ أَنَّهُمْ أَصْحَابُ الْجَحِيمِ}    التوبة:113}

"Haimpasii Nabii na wale walio amini kuwatakia msamaha washirikina, ijapo kuwa ni jamaa zao, baada ya kwisha bainika kuwa hao ni watu wa Motoni."      [Al-Tawba:113]

Na Allah ndie mjuzi zaidi

 

LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6575477
TodayToday184
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 11

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6829882f889389042147841747552303
title_6829882f88a4618989914791747552303
title_6829882f88b4c2959870761747552303

NISHATI ZA OFISI

title_6829882f8a47412538912271747552303
title_6829882f9c0a78771424171747552303
title_6829882f9c1bd13972653941747552303 Add content here

HUDUMA MPYA

: 9 + 8 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com