Menu

NI NINI UISLAMU?


WHAT


Uislamu ni dini ya mwisho ambayo amekuja nayo bwana Mtume Muhammad S.A.W na Uislamu umekuja kukamilisha sheria zote zilizopita. Na uislamu ni dini ya Mitume wote kwanzia Adam mpaka Mtume Muhammad .
Uislamu ni kunyenyekea na kujisalimisha kwa mungu na kumuabudu Mungu mmoja mwenye Nguvu alie Mbinguni.

MWENYEZI MUNGU NI NANI ?

Mungu au ALLAH ndie Mungu mmoja alieumba kila kitu na ndie anaeendesha kila kitu katika ulimwengu ni mungu mmoja anaejitegemea mwenye nguvu hakuzaa wala hakuzaliwa wala hafanani na kitu chochote wala haonekani kwa utukufu wake.

Mwenyzi Mungu anasema katika Qur'ani Tukufu Sura 112 Aya 1-4

[Sema: Yeye Mwenyezi Mungu ni wa pekee.Mwenyezi Mungu MkusudiwaHakuzaa wala hakuzaliwaWala hana anaye fanana naye hata mmoja.]


UISLAMU UNAFUNDISHA NINI?

Uislamu unafundisha kumuabudu mungu mmoja na kuacha kuabudu Masanamu na vitu vingine , Uislamu unafundisha Tabia njema, kuishi na Majirani vizuri, kuwatendea wema  wawili, na kuwafanyia wema watu wote hata wasiokua Waislamu imekuja katika Qur'ani Mwenyezi anasema:

[Hawakatazi Mwenyezi Mungu kwa wale wasiowapiga vita katika dini yenu na hawajawatoa katika majumba yenu kuwafanyia wema na kuwafanyia uadilifu hakika Mwenyezi Mungu anawapenda wenye kufanya uadilifu].   [60:8]

YESU NI NANI KWA WAISLAMU?

Yesu ama Nabii (Issa) ni binadamu kama binadamu wengine na ni Mtume katika Mitume wa Mwenyezi Mungu wala sio mungu wala mwana wa mungu na kuzaliwa kwake bila ya baba ilikua ni Miujiza katika miujiza ya mungu kwani yesu ni kama Nabii (Adam) ambae aliumbwa bila ya Baba wala Mama.

[Hakika mfano wa Isa kwa Mwenyezi Mungu ni kama mfano wa Adam; alimuumba kwa udongo kisha akamwambia: Kuwa! Basi akawa]     [3:59]

Na Nabii Issa au yesu kama Manabii wengine alipewa Miujiza ya kufufua maiti na kuwaponya wagonjwa sio kwa uwezo wake bali ni kwa uwezo wa Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho atawakana wanaomuabudu na sisi Waislamu tunaamini yakwamba yesu hakuuwawa wala hakusulubiwa bali alipaishwa Mbinguni kwa mwenyezi Mungu,na atashuka mwisho wa Dunia na kufariki.

[Na kwa kusema kwao: Sisi tumemuuwa Masihi Isa, mwana wa Maryamu, Mtume wa Mwenyezi Mungu - nao hawakumuuwa wala hawakumsalibu, bali walifananishiwa tu. Na hakika walio khitalifiana katika haya wamo katika shaka nayo. Wao hawana ujuzi nayo wowote, ila ni kufuata dhana tu. Wala hawakumuuwa kwa yakini Bali Mwenyezi Mungu alim- tukuza kwake, na hakika Mwenyezi Mungu ni Mwenye nguvu, Mwenye hikima.]  [4:157-158]


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6574326
TodayToday2393
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 14

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_6828db1d5a1227776890971747507997
title_6828db1d5a2988814032871747507997
title_6828db1d5a40f5030678001747507997

NISHATI ZA OFISI

title_6828db1d72d7a15851081041747507997
title_6828db1d72f3715374139461747507997
title_6828db1d730e120518307951747507997 Add content here

HUDUMA MPYA

: 11 + 4 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com