Menu

SOMO LA FIQHI


 somo lafiqhi


Suali: Madini ni nini? na inamanisha nini ya Hazina iliyozikwa ardhini?

Jawabu: Madini ni chochote kinachotolewa ndani ya ardhi ambacho kwamba sio sampuli ya ardhi kama vile dhahabu, fedha, vyuma, na vijiwe vya tunu kama vile almasi na rubi, na risasi, na vyenginevyo katika vitu asili vinavyotolewa ndani ya Ardhi.

Hazina iliyozikwa ardhini
Ni Mali iliyozikwa ndani ya ardhi kwa kuekwa na mtu, kutokana na dhahabu, na fedha, na mfano wa vitu hivi.

Suala: Ni ipi Hukumu ya zaka ya madini na hazina iliyozikwa ardhini
Jawabu: Hukmu yake ni lazima, kwa kauli ya Mwenyezi Mungu Mtukufu:

 

يَا أَيُّهَا الَّذِينَ آمَنُوا أَنفِقُوا مِن طَيِّبَاتِ مَا كَسَبْتُمْ وَمِمَّا أَخْرَجْنَا لَكُم مِّنَ الْأَرْضِ}   البقرة:267}

 

[Enyi mlioamini! Toeni katika vile vizuri mlivyovichuma, na katika vile tulivyokutoleeni katika ardhi] [Al-Baqarah: 267]

Na kauli ya Mtume ﷺ:

 

وفي الركاز الخمس]    رواه البخاري ومسلم]

 

[Na katika hazina iliyozikwa ardhini (toeni) khumusi (1/5))]   [Imepokewa na Bukharin a Muslim.]

Sauli: Ni yapi Masharti ya kutoa zaka ya hazina iliyozikwa ardhini
Jawabu: Hakuna masharti yoyote ya zaka ya hazina iliyozikwa ardhini, basi atakapomiliki mtu hio hazina iliyozikwa ardhini anafaa kutoa zaka yake moja kwa moja.

Kiwango cha kuwajibika mtu kutoa zaka ya madini na hazina iliyozikwa ardhini
Ni wajibu mtu kutoa khumusu (1/5) kwa kichache au kingi atakachopata katika madini na hazina iliyozikwa ardhini, kwa jumla ya kauli ya Mtume ﷺ:

 

وفي الركاز الخمس]  رواه البخاري ومسلم]

 

[Na katika hazina iliyozikwa ardhini (toeni) khumusi]     [Imepokewa na Bukhari na Muslim.]


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6575425
TodayToday132
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 23

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68297cca59c7811698938141747549386
title_68297cca59d607211177171747549386
title_68297cca59e526433569381747549386

NISHATI ZA OFISI

title_68297cca5b40f19305692551747549386
title_68297cca5b4f15990564861747549386
title_68297cca5b5df1639903891747549386 Add content here

HUDUMA MPYA

: 8 + 13 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com