Menu

SOMO LA FIQHI


somo lafiqhi


Aliye kwenye ihramu akisumukwa na Nywele tatu anapopangusa kichwa katika kutawadha au kuoga, hilo halimdhuru. Pia lau baadhi ya nywele za masharubu au ndevu zilisumuka au ukucha wake ukakatika, hilo halitamdhuru, isipokuwa akizisumua kwa kusudi. Na mwanamke analingana na mwanamume katika hilo la kutodhurika na kusumukwa na nywele au kucha.

Inafaa kwa aliye kwenye ihramu kufunga uzi mguuni mwake akihitajia hilo au kukiwa na maslahi ya kufanya hivyo.

UWEKAJI MASHARTI KATIKA NIA 

Ambaye ni mgonjwa, au anaogopea kutokewa na jambo lenye kumzuia kukamilisha ibada yake ya Hijja, ni sunna kwake aweke sharti wakati wa kuhirimia na aseme:

 

[لبيك عمرة، أو لبيك حجاً، "فإن حبسني حابس فمحلي حيث حبستني]

 

«Tunaitikia mwito wako wa Umra (au Hija) iwapo kutatokea kitu chochote chenye kunifunga mimi (nisimalize ibada yangu,) basi mahali pangu pa kutahalali ni pale uliponifunga».

Bibi Aishah radhi za Allah ziwe juu yake amepokewa akisema kwamba Mtume wa Mwenyezi Mungu aliingia kwa Dhuba'ah binti Zubair akamwambia: (Huenda ulitaka kuhiji) Aksema: “Najikuta naumwa. Akamwambia:

 

حجي واشترطي وقولي : اللهم محلي حيث حبستني]     رواه البخاري ومسلم]

 

[Hiji na ujiwekee sharti na useme ‘ Ewe Mola! Mahali pangu pa kujifungua na ihramu ni pale uliponifunga]  [Imepokewa na Bukhari na Muslim.].

Akisema hivyo, kisha akapatikana na jambo la kumzuia, basi itafaa atahalali (ajifungue na ihramu) bila kulazimiwa na kitu.


LOGOISLAM

Search Videos

RSS Content

<

 

WhatsApp This Page Now
 

Visitors Counter

6575090
TodayToday3157
Highest 01-07-2025 : 4073
US
Guests 9

Mkurugenzi na naibu wake

SS10

 

VIKAO VYA OFISI

title_68292b0f75ed810751900591747528463
title_68292b0f7600b21259063911747528463
title_68292b0f761403287344261747528463

NISHATI ZA OFISI

title_68292b0f8aa9a21150998271747528463
title_68292b0f8ac025251154021747528463
title_68292b0f8ad9312677243901747528463 Add content here

HUDUMA MPYA

: 15 + 12 =

IslamChoice- Kiswahili

Ni mtandao mpya wa ulinganizi unao funza mafunzo ya dini ya kiislamu kuambatana na Qur'ani na Sunna za Bwana Mtumeﷺ zilizo sahihi‎ kwa ufahamu wa wema walio tutangulia.

UongofuUongofu.com